Posts

Showing posts from May, 2024
Image
Mkurugenzi wa Shirika la Uwiano wa Maendeleo Vijijini/IRDO Dr. Simon Chiwanga, ametembelewa na Idara ya Masomo ya Biashara katika Chuo Kikuu Mzumbe Mkurugenzi wa Shirika la Uwiano wa Maendeleo Vijijini/IRDO Dr. Simon Chiwanga, ametembelewa na Idara ya Masomo ya Biashara katika Chuo Kikuu Mzumbe na kutembelea ofisi za shirika, pamoja na miradi inayotekelezwa na shirika ambayo ni HIV Prevention Care and Support, DREAMS na FOSENI II (Food Security and Nutrition Improvement) kwa lengo la kuona ni maeneno gani ambayo yanaweza kuboresha zaidi ushirika wa Chuo Kikuu cha Mzumbe na Shirika la Uwiano wa Maendeleo Vijijini. Katika ziara hiyo timu ya Chuo Kikuu cha Mzumbe ilieleza kua imejifunza mengi sana kwenye miradi inayotekelezwa na shirika na wameona maeneo mengi ambayo yanaweza kuboresha zaidi uhusiano ulipo kati ya shirika na Chuo Kikuu cha Mzumbe kama vile:- Kushauri na kusaidia kwa namna gani bidhaa zinazotengenezwa na wanufaika wa mradi wa DREAMS zifike sokoni vile vile kutoa msaada wa ...
Image
  Klabu ya Kupambana na Kudhibiti Ukatili wa Kijinsia na Watoto iliyopo katika shule ya sekondari Mwalimu Nyerere kata ya Chipaka, Halmashauri ya Mji Tunduma iliyoanzishwa na Shirika la IRDO kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Momba Bahati Simchile - Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Polisi na Mkuu wa Dawati la Jinsia na Haki za Watoto wilaya ya Momba akiwa na Judith Mwalukoba, Mshauri wa Mabinti na Rose Luvanda, Afisa Rasilimali Watu kutoka Shirika la Uwiano wa Maendeleo Vijijini (IRDO) wakitoa elimu na kushiriki michezo mbalimbali lengo ikiwa ni kupambana na kudhibiti ukatili wa kijinsia na kutetea haki za watoto kwenye Klabu ya Kupambana na Kudhibiti Ukatili wa Kijinsia na Watoto iliyopo katika shule ya sekondari Mwalimu Nyerere kata ya Chipaka, Halmashauri ya Mji Tunduma iliyoanzishwa na Shirika la IRDO kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilaya ya Momba inayowalenga watoto wa kike na kiume waliopo shuleni ili kuwasaidia kuelewa na kupambana dhidi ya ukatili wa kijinsia na...
Image
Mafunzo ya Uwezeshaji Kiuchumi kwa Wasichana Balehe na Wanawake Vijana Mafunzo ya Uwezeshaji Kiuchumi kwa Wasichana Balehe na Wanawake Vijana (wenye umri wa miaka 15 hadi 24) yaliyofanyika katika Kata ya Majengo, Halmashauri ya Mji wa Tunduma, Mkoa wa Songwe yaliyowezeshwa na IRDO kupitia mradi wa DREAMS kwa ufadhili wa HJFMRI. Katika mafunzo haya, washiriki walijifunza maarifa ya utengenezaji wa sabuni ya unga, mafuta ya mgando, na ubuyu ikiwa ni jitihada za kuboresha hali zao za kiuchumi kupitia fursa mbalimbali za ujasiriamali. Picha za tukio  
Image
Wanufaika wa mradi wa DREAMS (wenye umri wa miaka 15-24) wamekamilisha mafunzo yao ya cherehani katika kituo cha mafunzo kilichopo Chapwa-Tunduma TC. Mafunzo hayo yalianza tarehe 7 Februari 2024 na yalihitimishwa tarehe 7 Mei 2024.