Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika Mkoa wa Songwe: Shirika la IRDO Lajivunia Kuunga Mkono

Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika mwaka huu yamefanyika kwa kishindo katika Mkoa wa Songwe, yakishirikisha watoto, wananchi, na wadau mbalimbali. Shirika la IRDO lilikuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha tukio hili linafanikiwa na kutoa mchango wake kwa jamii. Katika viwanja vya Shule ya Sekondari Kakoma, wafanyakazi wa Shirika la IRDO pamoja na vijana wanaojitolea katika shirika hili walikusanyika kwa ajili ya kusherehekea siku hii muhimu. Huku wakiwa na furaha na shauku, walishirikiana na watoto na jamii kwa ujumla katika kuhamasisha haki za watoto, elimu bora, na ustawi wa watoto wetu. Katika tukio hili, vijana wanaojitolea katika shirika la IRDO waliweza kuwaelezea wadau na wananchi mbalimbali waliotembelea banda la shirika hilo kuhusu miradi inayotekelezwa na bidhaa zilizozalishwa na wanufaika wa miradi hiyo. Hili lilisaidia kutoa mwanga zaidi juu ya kazi nzuri inayofanywa na shirika katika jamii. 🌟🛍️🌱 Kwa kuzingatia umuhimu wa afya ya wasichana, wafanyakazi wa Shi...